King sports world wide.

Breaking News
recent

Vituko Yanga; Inonga arudisha mkwanja Yanga, amkimbia Mayele Airport

 

Inonga anasema kabla ya kuhitajika na Simba, Yanga walikuwa wa kwanza kumtafuta na kuna mmoja wa viongozi aliongea naye tena na mazungumzo yalifika mbali kwa kukubaliana kila kitu.

Anasema akiwa katika hatua za mwisho kufanya uamuzi Yanga alipokea simu kutoka kwa kiongozi mwingine wa juu wa Simba ambaye naye alimueleza kuhitajika katika timu hiyo huku wakimuwekea maslahi makubwa mezani kuliko yale ya Yanga.

“Nikiwa katika tafakari ya kufanya uamuzi tena muda huo nikiwa nimepima mpaka Uviko 19 na pesa iliyotumwa na Yanga, nilifanya mawasiliano na wachezaji wa DR Congo waliokuwa hapa nchini,” anasema Inonga na kukiri kwamba baada ya kufika nchini alilazimika kurejesha fedha za Yanga walizomtumia kulipia gharama za kupima Uviko. Kuhusu tiketi ambayo Yanga walikuwa wamemtumia anasema kwamba hakulazimika kuilipa kwavile hakuitumia, alisafiria tiketi ya Simba kuja Dar es Salaam. “Katika kufanya mawasiliano wenzangu waliokuwapo hapo na hata waliowahi kucheza waliniambia Simba ni bora kuliko Yanga kwa wakati ule, kwa hiyo nilibadili uamuzi na kuamua kutua Msimbazi.”

Inonga anasema Yanga walifanya kila kitu kwa ajili yake na walikuwa wanamsubiri nchini ili kuja kumalizana nao kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili.

“Dah! Nadhani ilikuwa imepangwa tu nije kucheza Simba kwani nilifika mpaka uwanja wa ndege wa Kinshasa ili nije Tanzania, lakini hilo lilishindikana na nilibadili uamuzi na kuja siku nyingine kwa ajili ya Simba,” anasema.

“Sikuweza kupokea wala kuwasiliana tena na Yanga baada ya siku niliyotakiwa kuja nchini kwa ajili yao kushindwa kufanya hivyo na nadhani wao walikuja kuona tu natambulishwa Simba.

“Haukuwa uamuzi rahisi kwani nilifika mpaka uwanja wa ndege, ila kutokana na sababu za msingi niliamua tu kubadili ule wa awali na kufanya uamuzi ya pili kuja katika kikosi cha Simba.”

Je, Alimkimbia Mayele?


Inonga anasema wakati anatakiwa kuja Tanzania kujiunga na Yanga walikuwa na tiketi sawa za ndege na Fiston Mayele na wote walikutana uwanja wa ndege kabla ya kuingia ndani.

Anasema wakati mwenzake akimtangulia ndani kukaguliwa ndipo alipobadili uamuzi baada ya kupokea maelekezo kutoka kwa msimamizi wake pamoja na Simba kwani walijua angetua na Mayele biashara ingemalizikia Jangwani.

“Kama unakumbuka ile mechi ya Yanga nilicheza kwa ushindani mkubwa dhidi yake na kuhakikisha hawezi kuleta hatari yoyote langoni kwani ni straika mzuri mwenye uwezo wa kufunga,” anasema Inonga.

“Mbali ya hivyo tumejuana tangu Congo kwa maana hiyo lazima kulikuwa na ushindani kati yetu kila mmoja akitaka kuisadia timu yake kushinda, lakini mbali ya masihara yetu pale uwanjani pamoja na ushindani mwisho wa mechi tuliongea na maisha mengine kuendelea.”


ARCH-FORUM TZ

ARCH-FORUM TZ

No comments:

Post a Comment

Google ads

Powered by Blogger.